Saturday, August 4, 2012

NGASA ATAKIWA KUJITUMA KUONYESHA KUWA YEYE NI BORA

Mrisho Ngasa akifika Coco Beach kwa ajili ya mazoezi na timu yake mpya

Ngasa akiwa mazoezini

Richard Amatre

Kocha msaidizi  wa klabu ya soka ya simba ya jijini dar es saam ambao ni mabingwa wa ligi kuu soka tanzania bara richard amatre  amemtaka mchezaji mpya wa timu hiyo waliyemsajili kutoka kutoka klabu ya Azam FC Mrisho Khalifani Ngasa kujituma na kudhihirisha kwamba yeye ni bora.

Kocha huyo ameyasema hayo wakati wa mazoezi ya klabu hiyo yanayofanyika katika fukwe za coco beach jijini dar es salaam. 

Amatre ambaye ni raia wa uganda amesema ngasa ni mchezaji mzuri na mwenye uwezo mkubwa sana wa kusakata kabumbu , hivyo  anatakiwa  kutilia makazao mazoezi kuhakish a anajituma kwa maslahi ya timu yake ya simba ili kuondoa dhana iliyojengeka katika vichwani mwa watu kwamba ana mapenzi zaidi na mahasimu wa klabu hiyo klabu ya yanga ya jijini dar es salaam.

Klabu ya soka ya azam fc ilifkia uamuzi wa kumuuza mchezaji huyo kufuatia uamuzi wa mchezaji huyo kubusu jezi ya timu yake ya zamani ya yanga  katika mchezo wa nusu fainali ya kombe la kagame iliyozikutanisha timu za Azam FC na AS Vita ya kutoka Jamhuri ya kidemokrasia ya kongo.

No comments:

Post a Comment