Kaze Cedri - Kocha wa Atletico |
Makocha wa timu za Tusker na Atletico zinazoshiriki michuano ya
Klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati Kagame wamesema ukiondoa timu za EL
salaam Wau ya Sudan na Ports ya Djibout timu zilizobakia yeyote inaweza kutwaa
kombe hilo.
Makocha hao ambao ni Kaze Cedrio wa Atletico ya Burundi
na Sam Omolo wa timu ya Tusker kutoka nchini Kenya wamesema hayo katika uwanja
wa Taifa jijini Dar es salaam.
Kocha Cedrio ameongeza kuwa licha ya kuwa timu nyingi
zimejiandaa vema lakini wachezaji wake wakijitahidi na kufuata maelekezo
anayoyaeleza ana imani mwaka huu kombe hilo litaenda nchini Burundi.
Sam Omolo –kocha mkuu wa Tusker |
Kwa upande wake kocha Sam amebainisha kuwa timu zimejiandaa
vizuri lakini timu itafanya vizuri maana ni timu nzuri na pia itaonyesha
changamoto.
Jumla ya timu 11 zimeshiriki michuano hiyo kutoka ukanda wa
Afrika ,Mashariki na kati CECAFA ambapo inafanyika kwa mara ya pili mfululizo
nchini Tanzania huku Yanga ikiwa ni Bingwa mtetezi wa kombe hilo.
No comments:
Post a Comment