Friday, July 20, 2012

BFT YATAKA MIKOA ICHAGUE MABONDIA WENYE VIWANGO KWA AJILI YA MASHINDAYO YA UBINGWA TAIFA


Shirikisho la ngumi za ridhaa tanzania BFT limeitaka mikoa kuchagua mabondia wenye viwango watakaoshiriki mashindano ya ubingwa taifa yanatarajiwa kuanza agosti 25 hadi 30 mwaka huu jijini dar es salaam.

Katibu mkuu wa BFT makore mashaga amesema kila mkoa unatakiwa kutafuta bingwa ambaye atakidhi viwango na kwamba ni vyema viongozi waliopewa jukumu la kuchagua mabingwa waangalie vigezo vinavyostahili.

Mashaga amesema ili timu ya taifa iweze kupata mabondia wazuri ni lazima viongozi waangalie uwezo wa wachezaji ambao watakuja kuliwakilisha vema taifa katika mashindano ya kimataifa.


No comments:

Post a Comment