Saturday, July 28, 2012

MATARAJIO YA WATANZANIA OLYMPIC 2012

Washiriki wa Olympic kutoka Tanzania
Baadhi ya waandishi waandamizi wa habari  wa michezo nchini wameoenyesha wasiwasi wa kufanya vema kwa wanamichezo kutoka nchini wanaoshiriki michuano ya olimpiki inayoendelea jijini London kutokana na maandalizi yasiyokuwa endelevu kwa wanamichezo mbalimbali.

Tanzania ni miongoni mwa nchi 204 zinazoshiriki mashindano hayo makubwa zaidi dunuiani katika michezo ya Ngumi Kuogelea na Riadha.

Ni katika hafla ya fupi ya kusheherekea kuanza kwa michuano hiyo iliyowakutanisha baadhi ya waandishi wa habari za michezo bega kwa bega na futari iliyondaliwa na kampuni ya Multchoice Tanzania kwa waandishi wa habari za michezo nchini ndipo suala la kutokuwa na imani na timu hiyo lilipoibuka.

Nao baadhi ya waandishi wa habari za michezo wamekuwa na maoni  tofauti, wapo wanaoamini kuwa wanamichezo hao watafanya vema huku wengine wakiweka bayana kamwe medali haziwezi kupatikana kutokana na aina ya maandalizi yaliyofanyika.

Aidha kwa upande wake Barbara Kambogi, Afisa habari wa Multichoice ametoa rai kwa watanzania kuwapa nafasi wanamichezo hao kwa kuamin kuwa watafanya vema.
 
Katika mchezo wa Ngumi Tanzania inawakilishwa na Suleiman Kidunda anayepigana Uzito kilo 64, Zakia Mrisho anayekimbia Riadha mita 1, 500, Msenduki Mohamed, Faustine Mussa, Samson Ramdhani wao watakimbia riadha nusu marathoni yaani kilomita 21.
 

No comments:

Post a Comment