Friday, July 27, 2012

MCHUMIA TUMBO AJITOKEZA KUPAMBANA NA AWADHI TAMIMU




Alfonce Mchumiatumbo


Bingwa wa ngumi za kulipwa za uzito wa juu hapa nchini Alfonce Mchumia Tumbo amesema yupo tayari kupambana na Awadhi Tamimu muda wowote na sehemu yeyote endapo atatokea promota wa kuandaa pambano hilo.

Bondia huyo anayeinukia hivi sasa katika masumbwi ameibuka na tambo hizo baada ya   tetesi kuwa Tamimu amekosa mpinzani wa kupambana nae ili kutetea mikanda anayoishikilia.

Mchumia tumbo ambaye kwa siku za hivi karibuni amekuwa akikimbiwa na baadhi ya mabondia pamoja na kusaini makubaliano ya kupambana nae amesema kwa sasa haoni  bondia mwenye uwezo wa kupanda nae ulingoni  zaidi ya Awadhi Tamimu ambaye kwa sasa anaishi Sweden.

Akizungumza kwa kujiamini mbele ya waandishi wa habari Mchumia Tumbo ameitaka kamisheni ya ngumi za kulipwa Tanzania TPBC kuandaa haraka iwezekanavyo pambano hilo ili aweze kumvua Tamimu mikanda yote ya uzito wa juu anayoishikili.

Alfonce Mchumia Tumbo ambaye ni mzaliwa wa mkoani Mbeya anashika nafasi ya kwanza Tanzania na kwa viwango vya dunia nafasi ya 317 amepanda ulingoni mara 7 ameshinda mapambano 6 yote kwa KO ametoka sare mchezo mmoja na hajapoteza pambano lolote.

Na Hassan Mvula

No comments:

Post a Comment