Timu za Azam FC na Yanga zimeingia katika fainali za kombe la Kagame ambapo watapambana katika mchezo wa kufa na kupona hapo jumamosi Julai 28 mwaka huu.

AS Vita na APR watakutana siku ya Jumamosi pia kuwania nafasi ya mshindi wa tatu.
Yanga ambao ni mabingwa watetezi wanayo kazi kubwa kutetea kombe hilo lisiende mikononi mwa wanalambalamba. Hata hivyo timu ya Azam FC imeonyesha kiwango kikubwa toka kwanzia msimu wa ligi kuu uliopita mpaka mashindano haya ya klabu bingwa za Afrika Mashariki na Kati CECAFA.
No comments:
Post a Comment