Makao makuu ya klabu ya Yanga Dar es Salaam |
KUFUATIA uchaguzi wa viongozi wa klabu ya Yanga unatarajiwa
kufanyika kesho katika ukumbi wa Diamond Jubilee Jijini Dar es Salaam uongozi
wa yanga na wanachama wa matawi mbali mbali kutoka Tanzania bara na Visiwani
wametoa maoni yao kuhusu uchaguzi huo.
Uchaguzi huo unafanyika kufuatia kujiuzulu kwa aliyekuwa
mwenykiti wa klabu hiyo Lyoid Nchunga na makamu wake Davis Mosha na baadhi ya
wajumbe wa kamati ya utendandaji wa Yanga.
Selestine Mwesigwa - Katibu Mkuu Yanga |
Katibu mkuu wa klabu hiyo Selestine
Mwasigwa amewataka wanachama wa klabu ya Yanga kujitokeza kwa wingi kushiriki
uchaguzi huo na kuchagua viongozi wanaofaa kuongoza klabu hiyo.
Wakati huu timu ya Yanga imefunguwa mashindano ya CECAFA Kombe la Kagame kwa kuchuana vikali na timu ya Atletico ya Burundi. Mpaka sasa kipindi cha pili dakika ya 85 timu ya Atletico imefunga goli moja na Yanga haijapata kuziona nyavu za Atletico
No comments:
Post a Comment